HABARI: NI MAJONZI MAZISHI YA MASOGANGE BELLE 9,ANT EZEKIEL,SEPETU,JACK WALPER,JOHN MWAKIPESILE,BILL NAS WAHUDHULIA

√√ Leo ilikuwa siku ya simanzi katika jiji la mbeya Baada ya mwili wa aliyekuwa msanii wa bongo movie na video exen(video queen ) maarufu nchini AGNESS JERALD (MASOGANGE ) kuwasili nyumbani kwao Mbalizi jijini mbeya kwaajili ya mazishi ukitokea Dar es salaam alikopatwa na umauti ijumaa week iliyopita.
          Aidha katika mazishi hayo yalihudhuriwa na wasanii mbalimbali wa bongo flavour,bongo movie,Gospel pamoja na viongozi wa serikali wakiwemo BELLE 9,ANT EZEKIEL,WEMA SEPETU,JACKLINE WALPER,JOHN MWAKIPESILE (Gospel ) Bill NASS,DOGO JANJA pia viongozi mbalimbali wa serikari wakiongozwa na Mkuu wa mkoa wa Mbeya AMOSI MAKALA,mkuu wa wilaya ya Mbeya pamoja na kamanda wa polisi Mkoa.

               AGNESS GERARD WAYA AU MASOGANGE alizaliwa 1989 kata ya Utengule,Mbalizi mkoani Mbeya na alifariki 20/04/2018 katika hospital ya MAMANGOMA jijini Dar.MASOGANGE (jina hili lilitokana na video aliyoshiriki ya msanii maarufu wa bongo flava BELLE 9 iliyojulikana kama MASOGANGE )
           Msanii huyu ameacha mtoto mwenye miaka 11 anayesoma darasa la saba.
          ^^Kwa pamoja tunasema BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LAKE LIBARIKIWE

             ®Gospel star newz tz 2018
  0712688802

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

SAMUEL MV BUKOBA KUZINDUA NANI ANIFUTE MACHOZI

NANI NI NANI? YOHANA MGAYA(MASANJA JUNIOR)

GOODLUCK GOZBERT AACHIA VIDEO HAUWEZI KUSHINDANA